Global Publishers
April 7, 2026
0 Comments
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameungana na viongozi wengine wa serikali na chama katika kuadhimisha Siku ya Kumbukumbu ya Karume Day kwa kufanya heshima maalum ya kuweka shada la maua katika kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Hayati Abeid Amani Karume.
Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 07, 2026, mara baada ya dua maalum iliyosomwa katika Afisi Kuu ya Chama cha Mapinduzi iliyopo Kisiwandui, Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu na heshima kwa mchango mkubwa wa Hayati Karume katika historia ya nchi na maendeleo ya Zanzibar.
Viongozi mbalimbali pamoja na wananchi walihudhuria tukio hilo, wakikumbushwa umuhimu wa kudumisha amani, umoja na mshikamano uliojengwa na waasisi wa taifa. Karume Day huadhimishwa kila mwaka kama njia ya kumuenzi na kutambua mchango wake katika mapinduzi na uongozi wa Zanzibar.




