DKT, KISENGE ;UVUTAJI WA SIGARA NA SHISHA UNACHANGIA ONGEZEKO LA UGONJWA WA MOYO

………

Na Ester Maile Dodoma 

Taasisi ya Moyo ya Jakaya kikwete  imeandaa kampeni ya ijue namba yako ,kwa lengo la kuwataka wananchi kùweza kujua mapigo yao ya moyo ,sukari ,na mafuta yaliyopo mwilini kwa kupima afya zao mara kwa mara na kufanya mazoezi ili kupunguza changamoto la tatizo la moyo .

Amezungumza hayo Mkurugenzi Mkuu  wa taasisi hiyo Dk. Peter Kisenge wakati akizungumza na waandishi wa habari leo 9 Aprili jijini Dodoma wakati akitoa mafanikio yaliyopo katika  taasisi  hiyo. 

Aidha Dk Kisenge amesema vifo vingi vinavyotokea vinatokana na tatizo la moyo ambapo kwa asilimia kubwa linawapata wanaume huku ikielezwa chanzo kikubwa ni mitindo wa maisha,huku akitaja  uvutaji wa sigara na sisha kusababisha tayizo hilo.

Hata hivyo taasisi  ya Moyo ya Jakaya kikwete imeandaa  mfumo maalumu wa upandikizaji wa  moyo ambapo itaenda kuokoa maisha ya watanzania wengi .