TMA yatoa tahadhari ya mvua kubwa, wananchi waonywa
Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa ya tahadhari na angalizo la mvua kubwa kwa mikoa kadhaa, ikisisitiza kuwa wananchi wanapaswa kuchukua tahadhari stahiki ili kuepuka madhara yanayoweza kutokana na hali ya hewa mbaya. Katika taarifa hiyo, TMA imetahadharisha kuwa Ijumaa ya Machi 20, 2026, kunatarajiwa kuwa na mvua kubwa…