Ajira 1,300 za kada ya afya zanukia Zanzibar
Unguja. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetangaza mpango wa kutoa ajira 1,300 kwa wataalamu wa sekta ya afya, katika jitihada za kukabiliana na upungufu wa watumishi na kupunguza msongamano katika hospitali za rufaa. Hatua hiyo inatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa, huku wataalamu hao wakipangiwa kufanya kazi zaidi katika zahanati na vituo vya afya, ambako…