Rithe: Tutaadhimisha mwezi wa wanawake kwa kuwakumbuka waliopoteza maisha Oktoba 29, 2025
Dar es Salaam. Ngome ya Wanawake ya Chama cha ACT-Wazalendo imetangaza kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, pamoja na mwezi mzima wa Machi, kwa kuwakumbuka waliopoteza maisha wakati wa vurugu zilizotokea katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025. Vurugu hizo zilisababisha vifo vya watu kadhaa, majeruhi na uharibifu wa mali za umma na binafsi. Aidha, zilisababisha…