Wajane Rukia na Habiba, wanaopambana na mawimbi kutafuta riziki
Dar es Salaam. Jua la asubuhi linaanza kuchomoza juu ya ufukwe wa Kawe Beach, mawimbi yakigonga kwa utulivu mchanga wa bahari. Ni katika eneo hilo ninaposubiri kwa zaidi ya saa tatu, nikitazama kwa makini kina cha maji ambako wavuvi wamezagaa wakitafuta riziki. Lakini kati ya wote waliopo baharini, macho yangu yanavutiwa zaidi na wanawake wawili…