Mbinu mpya uingizaji wa mihadarati zinatia hofu

Biashara haramu ya dawa za kulevya inaendelea kubadilika kadiri mamlaka zinavyoimarisha udhibiti wake. Hivi sasa, wafanyabiashara wa dawa hizo wamebuni mbinu mpya ya kuziingiza Zanzibar, hali inayoongeza wasiwasi kuhusu usalama wa jamii, hususan watoto na vijana. Mbinu hii mpya imeibuka baada ya njia nyingi zilizokuwa zikitumiwa kwa muda mrefu, zikiwemo kuzimeza na kuzibeba tumboni, kugundulika…

Read More

TUONGEE KIUME: Tuheshimu kiapo cha ndoa, talaka si ujanja

Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na wimbi la kusikitisha la kuvunjika kwa ndoa nchini, huku takwimu zikionyesha kuwa wanaume wengi wameanza kuichukulia talaka kama jambo la kawaida au fasheni. Tofauti na zamani ambapo talaka ilionekana kuwa ni jambo la mwisho na la dharura baada ya jitihada zote kushindikana, leo hii imekuwa ni kama “mazoea”…

Read More

Waziri Mkuu Asisitiza Amani, Maadili Na Ushirikiano Na Taasisi Za Dini – (Picha +Video)

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi za dini nchini katika kulinda amani, kuimarisha maadili na kuchochea maendeleo ya Taifa. Dkt. Mwigulu amesema hayo leo Jumapili (Machi 15, 2026) wakati akitoa salamu katika Ibada iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Mpanda Mjini, Dayosisi ya…

Read More

Mambo 7 yamkalia pabaya Pedro Yanga

YANGA inaendelea kugawa dozi kwenye mechi zake ikitoka kupata mshtuko wa kudondosha pointi mbili baada ya kulazimishwa sare dhidi ya Simba, mchezo ambao uliibua hoja mbalimbali juu ya kiwango cha kikosi hicho. Huo ulikuwa mchezo wa kwanza wa dabi timu hiyo ikiwa chini…

Read More

Siku ya Ushindi na Meridianbet Imefika

WAKALI wa ubashiri wanakuita leo hii usuke jamvi lako la ushindi sasa. Timu kibao zipo uwanjani leo kusaka ushindi na wewe ingia kwenye akaunti yako ya Meridianbet usake mkwanja sasa. EPL leo hii itaendelea Arsenal atakuwa nyumbani kukiwasha dhidi ya Everton ambao wanashika nafasi ya 8 kwenye msimamo w aligi. Wageni wao wapo nafasi ya…

Read More

Safari ya wanaanga wa NASA; Rekodi, sayansi na historia

Dar es Salaam. Wanaanga wanne kutoka Shirika la Anga la Marekani (NASA) wameanza kurejea duniani baada ya kukamilisha safari ya kihistoria ya kuuzunguka mwezi, na kufanikiwa kufika mbali zaidi na Dunia kuliko binadamu yeyote kuwahi kufika. Safari hiyo ya siku 10, iliyoanza Aprili mosi, 2026, iliyopewa jina ‘Artemis II’, imehusisha wanaanga Reid Wiseman, Victor Glover,…

Read More

Vikwazo kwa zao la tende vyawekwa hadharani, wanaume wakitajwa kuongeza thamani

Dodoma. Changamoto ya upatikanaji wa miche bora ya tende pamoja na masharti yanayowekwa na nchi zinazolima zao hilo zimetajwa kuwa miongoni mwa vikwazo vinavyokwamisha ukuaji wa kilimo cha tende nchini. Kutokana na vikwazo hivyo, wakulima wengi wameendelea kutumia mbegu za zamani, ambazo zinaelezwa kuwa hazina tija katika kipindi hiki. Hali hii inajitokeza wakati mahitaji ya…

Read More

Vyombo vya ukandamizaji vya Jimbo la Venezuela ‘zisizobadilika’ licha ya mabadiliko ya uongozi – Masuala ya Ulimwenguni

“The miundo ambayo imeendeleza mateso kwa miaka mingi haijavunjwa, wala sera za Serikali hazijatangazwa kuanza mchakato huo.”, Ujumbe wa Kimataifa wa Kutafuta Ukweli kwa Venezuela ulisema katika a taarifa iliyotolewa Jumatano. Ujumbe huo ulianzishwa ili kutathmini madai ya ukiukaji wa haki za binadamu nchini Venezuela uliofanywa tangu 2014. Tangu kukamatwa kwa Maduro mnamo Januari 3,…

Read More