CCM K’njaro yatoa kauli viongozi 70 kusaini kumkataa kigogo, kutishwa
Dar es Salaam. Wakati msuguano ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Moshi Mjini ukiendelea kushika kasi ikiwamo viongozi 70 kusaini barua ya kutokuwa na imani na kigogo wa chama hicho ngazi ya wilaya, Mkoa wa Kilimanjaro umesema inafanyia kazi madai yote na hatua zitachukuliwa. Taarifa za uhakika zilizolifikia Mwananchi, zinaeleza miongoni mwa waliosaini…