DKT TULIA AZINDUA JEZI YA BETIKA MBEYA TULIA MARATHON 2026

KAMPUNI Ya ubashiri ikishirikiana na Taasisi ya Tulia trust kupitia Betika Mbeya Tulia Marathon imezindua rasmi jezi ambayo itatumika Msimu wa 10 wa Mashindano Jijini Mbeya mwaka huu.

Akizungumza na Wanahabari  Jijini Dar es Salaam Meneja Mkuu wa Betika Tanzania Samuel Mcheru amesema Betika inathamini sana michezo na itaendelea kutoa ushirikiano mkubwa kupitia Taasisi ya Tulia trust Kuhakikisha mbio hizo za Betika Mbeya Tulia Marathon zinafanyika kwa ufanisi mkubwa .

Hata hivyo ameongeza kuwa mashirikiano hayo yanalenga kuwaweka wananchi karibu na kushiriki michezo ili kuweka miili yao imara zaidi,kurudisha tabasamu kwa jamii na kutoa fursa za kibiashara kwa Wananchi wa Jiji hilo.

Mcheru ametoa wito kwa Makampuni mengine yawe yenye tija katika jamii kwani uwepo wa Betika Tulia Marathon ni kiashiria tosha kuwepo kwa ongezeko la kipato kila inapofanyika kutokana na jamii kukusanyika eneo moja hivyo inawapa fursa betika pia kujitangaza zaidi na Wafanyabiashara kuendesha shughuli zao.

Kwa upande wake Mbunge wa Mbeya na Spika wa Bunge Mstaafu Dkt.Tulia Ackson amesema Kampuni ya Betika imekuwa na mchango mkubwa wa kuhakikisha mbio hizo zinafanyika kwa ufanisi mkubwa hasa kwa mchango wao wa vifaa vya kushiriki mbio hizo pamoja na miundombinu mbalimbali pindi linapokuja shindano hilo kutokana na kuweka udhamini wao kwa zaidi ya Miaka mitatu.

Ackson amesema kwa mwaka huu shindano hilo linatimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake na kwa mwaka huu wanategemea kukusanya kiasi cha fedha shilingi milioni 300 ili kugusa Maeneo ya Kijamii mbalimbali ikiwemo Kuboresha makazi ya Wahitaji, eneo la Afya hususani kujenga baadhi ya wodi hitajika, vifaa pamoja na eneo la Elimu Mashuleni.

Hata hivyo amesema Mbio hizo za kipekee zilizopewa chachu na hali ya hewa ya jiji hilo itatimua vumbi Mei 15 na 16 zikiambatana na burudani mbalimbali.

Aidha amevipongeza vyombo vya habari kwa kuendelea kutoa habari juu ya Taasisi ya hiyo ambayo kutokana na michango ya wadau mbalimbali katika kujikita kusaidia jamii.

Pia ametoa wito kwa Watanzania kujiandikisha kushiriki katika mbio hizo kupitia Ofisi zilizopo Jijini Mbeya pamoja na kujisajili mtandao kwenye kurasa za Taasisi hiyo.

Nae Afisa Habari wa Kampuni ya Betika Juvenalius Rugambwa aliongeza kuwa Jezi hiyo iliozinduliwa itatumika rasmi kwenye mbio hizo huku akisherehesha kuwa jezi hizo zimepambwa na rangi zenye mvuto zaidi zenye michoro ya vivutio vilivyopo Tanzania ikiwemo bendera ya Taifa .